Tamthilia ya Kicheko cha Dhiki inachora taswira kamili ya mataifa mengi ya Kiafrika.Wananchi wa taifa la Sinzia wanashuhudia kuzorota kwa uongozi wa Mtemi Zedekaya. Fursa mpya ya kuchagua Mtemi mpya imebakia mikononi mwa wananchi hao. Je, vijana watapata nafasi ya kuongoza Sinzia? Je, Mtemi Zedekaya atabakia kuwa kiongozi wa Sinzia? Je, viongozi waliounga mkono Mtemi Zedekaya watampenda tena?
Tamthilia hii imemulika hulka ya viongozi waliochaguliwa debeni, asasi ya ndoa, nafasi ya vijana na kina mama katika jamii,na idara ya usalama kwa jumla. Suala la dini, ajira na ndoa limepigwa msasa. Mwandishi ana imani kuwa utagundua maudhui mengine, upate kuelimika ,na kuburudika.
Reviews
There are no reviews yet.