Kichele Cha Ushairi ni diwani iliyoandikwa kwa kuzingatia mtaala wa kiumilisi wa Gredi ya saba nane na ya tisa kutoka Taasisi ya Ukuzaji Mitaala Nchini Kenya (KICD). Diwani hii ipo kwa madhumuni ya kuwasaidia wanafunzi kuwa na uelewa na uchambuzi wa mashairi. Mashairi pamoja na matini yameandikwa kwa lugha nyepesi yenye uelewa wa haraka. Mashairi hayo yametungiwa maswali ainati ya kumpa mwanafunzi ari ya kuyajibu. Katika maudhui, Kichele kimemulika jamii ya sasa kwa kuangazia masuala ibuka kwa nia ya kuwaelimisha, kutahadharisha, kuonyana kuwapa wanafunzi mbinu-ishi ya kukabiliana na hali mbalimbali inayomzingira. Kimsingi diwani hii imeshughulikia:
Maana ya shairi
Sifa za shairi
Umuhimu wa mashairi
Istilahi za kishairi
Aina za mashairi- kutegemea idadi ya mishororo katika beti
Mashairi mbalimbali yaliyo na maswali ya kuwakina wanafunzi kichwa.
Soma uchote maarifa.
Waandishi:
Duke Nyakundi (Mwalimu Nyakundi), Ann Mwanasarifu, Juliah Ngunu, Samson Matoke Nyamosi, Olando Joel Wanjala, Dennis Ngatia, Faustine Marie,Keziah Macharia, Henry Mong’are Moindi na Rashid Athuman Hamisi ni waandishi waliobobea katika ulingo wa ushairi. Wameandika kazi nyingi za Fasihi si riwaya, si tamthilia si hadithi fupi. Waandishi hawa wamejituma kwa sana kuhakikisha kuwa ujumbe umefika kwa jamii husika kwa lugha ya usahali.
Marie Faustine –
Kitabu murua hiki!